WAHITIMU WA SHULE YA MSINGI YA MAZOEZI CHANG’OMBE WAREJEA SHULENI KUTOA SHUKRANI
Wanafunzi wa zamani waliohitimu katika Shule ya Msingi ya Mazoezi Chang’ombe kuanzia mwaka 2000, wametembelea shule hiyo tarehe 7 Agosti 2026 kwa lengo la kutoa shukrani kwa walimu wao pamoja na kuwatia moyo na hamasa wanafunzi wanaosoma shuleni hapo kwa sasa.