Uongozi wa Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) unapenda kuwataarifu wanafunzi wote kuwa, kuanzia mwaka wa masomo 2026/2027, kutakuwa na viwango vipya vya tozo zinazolipwa moja kwa moja na wanafunzi pamoja na gharama za malazi katika mabweni na hosteli za Chuo. Viwango hivyo vinahusu, miongoni mwa mambo mengine, gharama za usajili, mitihani, huduma za TEHAMA na Maktaba, vitambulisho, nyaraka mbalimbali za kitaaluma, mahafali pamoja na huduma nyingine zinazohusiana na masomo. Gharama mpya za malazi katika mabweni na hosteli mbalimbali pia zimeainishwa kwa mwaka huo wa masomo.